Skip to main content

NI YEYE..MTUNZI ALLY KHELEF

 







       LEO,  Tutajifunza na kuburudika na utungaji wa mashairi ya kiswahili kutoka kwa mtunzi wetu Bwana ALI ABEID KHELEF......Karibu..!!

SHAIRI; NI YEYE

     Nazizima nikizani, cha kale kujitunzia, 

meingia mahabani, wavyele wanizuia, 

Nimpendae Fulani, mtima kauhamia, 

                     NI YEYE!!


Kwake yeye ni peponi, tayari nimeingia, 

Wazaziwe hawaoni, thamani kunipatia, 

Awe wangu wa ndoani, nusu dini kutimia, 

                    PINGAMIZI


Pendo langu mashakani, nahisi linapotea, 

Latanga tanga njiani, angani likielea, 

Kumkosa muhisani, moyo utanyong'onyea, 

                        MAUMIVU.!

Katika shairi hili fupi ambalo dhamira yake kuu ni tatizo kubwa ambalo watu mbali mbali huwakumba pale wanapoamua kwa moyo mkunjufu kuipalilia miti yao ya matunda lakin hukutana na vipingamizi kutoka kwa wazazi kutokana na sababu mbali mbali kama vile udini, ukabila, siasa, kipato, na mengine mengine ambayo hukata uzi wa pendo zito la wapendanao ambapo, wawili walioshibana hupelekea mifarakano ndani ya jamii.....na chuki endelevu zisizokwisha ndani yamii........TUBADILIKE...

Comments

  1. Mahaba kua makini,ndoani utajalia.
    Vishilingi mfukoni, visiwe vyakuzuzua.
    Watamani wa fulani, jipange utaumia.
    Ni maneno ya Thamani, zingatia na Tambua

    ReplyDelete
    Replies
    1. pendo kulitathmini, wengi hawajatambua,
      maneno yawe laini, laasivyo wapotea,
      kupenda si jambo geni, wa kwanza mimi sikuwa,
      sijamwona wa fulani, huru nilipo chagua,
      KAJUJU

      Delete
  2. Usiwe mtu auni, mwezako kumtishia,
    Hakuna wa fulani, ndoani hajaingia,
    Mwezako yupo tabani, kwa X ametulia,
    Kama fulani ni wko, ndoani ngeshamuweka.
    KAJUJU

    ReplyDelete
  3. Hujui ulisemalo, yafaa kulichungua,
    Nateta shika shikilo, tengua tena tengua,
    Kujua nilishikalo, yataka kufatilia,
    Pendo napima kwa kilo, wallahi nafurahia,

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

WRITING SKILLS - WRITING LETTER

  How to Write a Letter? Knowing how to write a letter, whether business or personal, is  a skill  we all need. Sometimes, these letters will be short and informal emails. Other times, they'll be highly polished for corporate correspondence. Below, we'll lay out the specific steps for letter-writing, explore some general tips, and review two specific types of letters. Writing a Letter Letter Writing A letter is a written message that can be handwritten or printed on paper. It is usually sent to the recipient via mail or post in an envelope, although this is not a requirement as such. Any such message that is transferred via post is a letter, a written conversation between two parties. Now that E-mails ( Advantages and disadvantages ) and texts and other such forms have become the norm for communication, the art of letter writing has taken a backseat. However, even today a lot of our communication, especially the  formal kind , is done via letters. Whether it is a cover letter f

10 COMMON SENTENCE MISTAKES IN ENGLISH

  Some mistakes are common when writing sentences in English. Each of these 10 common sentence mistakes provides correction information as well as links to more detailed information.  Incomplete Sentence or Sentence Fragment One  common mistake  many students make is the use of  incomplete sentences . Each sentence in English must contain at least a subject and a verb, and should be an independent clause. Examples of incomplete sentences without a subject or a verb might include an instruction or a  prepositional phrase . For example Through the door. In the other room. Over there. These are phrases we may use in spoken English. These phrases shouldn't be used in written English as they are incomplete.  Sentence fragments caused by dependent clauses used without an  independent clause  are more common. Remember that  subordinating conjunctions  introduce  dependent clauses . In other words, if you use a subordinating clause beginning with a word such as 'because, though, if, et