LEO, Tutajifunza na kuburudika na utungaji wa mashairi ya kiswahili kutoka kwa mtunzi wetu Bwana ALI ABEID KHELEF......Karibu..!!
SHAIRI; NI YEYE
Nazizima nikizani, cha kale kujitunzia,
meingia mahabani, wavyele wanizuia,
Nimpendae Fulani, mtima kauhamia,
NI YEYE!!
Kwake yeye ni peponi, tayari nimeingia,
Wazaziwe hawaoni, thamani kunipatia,
Awe wangu wa ndoani, nusu dini kutimia,
PINGAMIZI
Pendo langu mashakani, nahisi linapotea,
Latanga tanga njiani, angani likielea,
Kumkosa muhisani, moyo utanyong'onyea,
MAUMIVU.!
Katika shairi hili fupi ambalo dhamira yake kuu ni tatizo kubwa ambalo watu mbali mbali huwakumba pale wanapoamua kwa moyo mkunjufu kuipalilia miti yao ya matunda lakin hukutana na vipingamizi kutoka kwa wazazi kutokana na sababu mbali mbali kama vile udini, ukabila, siasa, kipato, na mengine mengine ambayo hukata uzi wa pendo zito la wapendanao ambapo, wawili walioshibana hupelekea mifarakano ndani ya jamii.....na chuki endelevu zisizokwisha ndani yamii........TUBADILIKE...
Mahaba kua makini,ndoani utajalia.
ReplyDeleteVishilingi mfukoni, visiwe vyakuzuzua.
Watamani wa fulani, jipange utaumia.
Ni maneno ya Thamani, zingatia na Tambua
pendo kulitathmini, wengi hawajatambua,
Deletemaneno yawe laini, laasivyo wapotea,
kupenda si jambo geni, wa kwanza mimi sikuwa,
sijamwona wa fulani, huru nilipo chagua,
KAJUJU
Usiwe mtu auni, mwezako kumtishia,
ReplyDeleteHakuna wa fulani, ndoani hajaingia,
Mwezako yupo tabani, kwa X ametulia,
Kama fulani ni wko, ndoani ngeshamuweka.
KAJUJU
Hujui ulisemalo, yafaa kulichungua,
ReplyDeleteNateta shika shikilo, tengua tena tengua,
Kujua nilishikalo, yataka kufatilia,
Pendo napima kwa kilo, wallahi nafurahia,